Baadhi ya waananchi waliowezeshwa mafunzJamiio ya ushonaji katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felister Mdemu alipotembeea kukagua uendeshaji wa miradi Chuoni hapo Oktoba 17,2025 Mkoani Iringa.
Naibu Katibu Mkuu wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felister Mdemu akiangalia mradi wa kufuga samaki alipotembelea Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha tarehe 16 Oktoba, 2025 mkoani Iringa.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu akiwa katika picha na Wazee wanaolelewa katika Makazi ya Wazee Wasiojiweza cha Tushikamane Pamoja Foundation yaliyopo Kata ya Kwembe, Manispaa ya Ubungo mkoani Dar Es Salaam tarehe 15 Oktoba, 2025 wakati wa ziara yake katika Makazi hayo .
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt John Jingu akipokea tuzo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mchango wake katika uboreshaji huduma za ustawi wa Jamii wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Ustawi wa Jamii katika Viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii Kijitonyama Dar Es Salaam Agosti 30, 2025.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt John Jingu akipokea tuzo ya Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mchango wake katika...wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Ustawi wa Jamii katika Viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii Kijitonyama Dar Es Salaam Agosti 30, 2025.
Washiriki mbalilmbali katika Wiki ya Ustawi wa Jamii iliyoanza kufanyika kuanzia tarehe 25 - 30 Agosti, 2025, katika Viwanja vya Taasisi ya Ustawi wa Jamii, Kijitonyama Dar Es Salaam
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akiwa na Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu Uanzishwaji wa Mfuko wa Pamoja wa Ruzuku kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NBF) katika Kongamano la Mwaka la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali 2025, Agosti 13, 2025, jijini Dodoma.
Watoto wakiwa katika maandamano katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika 2025 katika viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii Kijitonyama Dar Es Salaam Juni 17, 2025.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii. Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akiwasilisha bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Bungeni jijini Dodoma Mei 27, 2025
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima (Mb), akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia ziara rasmi ya Mhe. Rais Alexander Stubb wa Jamhuri ya Finland katika Soko la Machinga Complex jijini Dar Es Salaam, 16 Mei,2025