Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi MaryPrisca Mahundi akiwa katika picha na viongozi pamoja na wajumbe wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Jiji la Dodoma Novemba 28,2025
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum,Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, akivishwa skafu na watoto wa
Shule ya Msingi Martin Luther, mkoani Dodoma, Novemba 26, 2025, wakati alipowasili kuzungumza na watoto hao kuhusu matumizi ya mitandao na athari zake kwao kuelekea likizo ya mwisho wa mwaka.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima akiwa na Naibu wake Mhe. Mhandisi MaryPrisca mara baada ya kupokelewa na Menejmenti na Watumishi wa Wizara katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma tarehe 18 Novemba, 2025. Wengine ni Katibu Mkuu Dkt. John Jingu na Naibu Katibu Mkuu Wakili Amon Mpanju.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi MaryPrisca Mahundi akiwa katika picha na mmoja ya kikundi cha Malezi Mkoa wa Ddodoma mara baada ya kuzungumza na wanavikundi vya malezi na matunzo ya watoto Kata ya Ihumwa Jijini Dodoma tarehe 27 Novemba, 2025.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felister Mdemu (wa tatu kushoto) akiwa katika Mkutano Mkuu wa 21 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO’s General Conference) unaohitimishwa jijini Riyadh, Saudi Arabia, Novemba 27, 2025.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima (katikati), akiwa katika picha na Naibu wake Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi ( wa nne kushoto) , Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi na Vyo vya Maendeleo ya Jamii mara baada ya kikao na Watumishi wa Wizara hiyo kilicholenga la kuboresha utendaji kazi ili kuifikia Jamii na kuihudumia kwa kasi na ufanisi zaidi. Kikao hicho kimefanyika Novemba 25, 2025 Mtumba jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu akiwa katika picha ya pamoja na uongozi kutoka Shirika lisilo la Kiserikali linalosaidia watoto wasio kuwa na malezi ya wazazi na familia zilizo katika hatari (SOS CHILDREN'S VILLAGES) mara bbada ya Kikao hicho kilichofanyia tarehe 26 Novemba, 2025 katika Ofisi yake Mtumba Jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felista Mdemu akigawa hundi ya Shilingi Milioni 337 kwa wanufaika wa Mkopo wa Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF) tarehe 14 Novemba, 2025 katika ukumbi wa Wizara hiyo uliopo Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Mkaundi Maaalum Dkt. John Jingu, tarehe 24 Oktoba, 2025 amegawa pikipiki nane (8) kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wa ngazi ya kata mkoani Njombe huku akiwataka Maafisa Maendeleo ya Jamii Mkoani Njombe kutunza na kutumia kwa umakini pikipiki walizopewa na Serikali kwa ajili ya kuboresha utendaji na utoaji huduma kwa wananchi.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Wakili Amon Mpanju tarehe 24 Oktoba 2024 amekabidhi pikipiki nane (8) kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Geita kutpka Kata za Muganza, Kigongo, Lwamgasa, Shabaka, Uyovu, Namonge, Masumbwe na Lulembela katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa huo.