Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Makundi Maalum

KITENGO CHA MAKUNDI MAALUM

Lengo

Kuimarisha na kuhudumia Makundi Maalum yaliyotambuliwa wakiwemo Machinga kulingana na mahitaji yao; kwa kuzingatia Sera, Mikakati; Programu, Sheria, Kanuni na Miongozo.

Kitengo kitatekeleza shughuli zifuatazo:-

  1. Kufanya utambuzi wa kijamii ili kubaini Makundi Maalum, Mahitaji yao na Changamoto zao;
  2. Kupitia na kuhuisha Sera ya Maendeleo ya Jamii ili kuingiza masuala ya Makundi Maalum;
  3. Kuendeleza na kuboresha mfumo wa kuhifadhi taarifa za Makundi Maalum;
  4. Kubuni, kufuatilia na kutathmini programu zinazohusiana na Makundi Maalum;
  5. Kutambua, kuratibu, kusimamia na kufuatilia afua za Wadau zinazohusiana na Makundi Maalum;
  6. Kuandaa sheria, kanuni na miongozo ya Makundi Maalum;
  7. Kutoa suluhisho/mapendekezo ya kibunifu zinazohusu Makundi Maalum kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa;
  8. Kujenga uelewa kwa Makundi Maalum juu ya uzingatiaji wa sheria na kanuni zinazohusiana na shughuli zao; na
  9. Kuwezesha vikao vya Makundi Maalum ambavyo vitahusisha Wadau mbalimbali.