Makundi Maalum
Makundi Maalum
KITENGO CHA MAKUNDI MAALUM
Lengo
Kuimarisha na kuhudumia Makundi Maalum yaliyotambuliwa wakiwemo Machinga kulingana na mahitaji yao; kwa kuzingatia Sera, Mikakati; Programu, Sheria, Kanuni na Miongozo.
Kitengo kitatekeleza shughuli zifuatazo:-
- Kufanya utambuzi wa kijamii ili kubaini Makundi Maalum, Mahitaji yao na Changamoto zao;
- Kupitia na kuhuisha Sera ya Maendeleo ya Jamii ili kuingiza masuala ya Makundi Maalum;
- Kuendeleza na kuboresha mfumo wa kuhifadhi taarifa za Makundi Maalum;
- Kubuni, kufuatilia na kutathmini programu zinazohusiana na Makundi Maalum;
- Kutambua, kuratibu, kusimamia na kufuatilia afua za Wadau zinazohusiana na Makundi Maalum;
- Kuandaa sheria, kanuni na miongozo ya Makundi Maalum;
- Kutoa suluhisho/mapendekezo ya kibunifu zinazohusu Makundi Maalum kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa;
- Kujenga uelewa kwa Makundi Maalum juu ya uzingatiaji wa sheria na kanuni zinazohusiana na shughuli zao; na
- Kuwezesha vikao vya Makundi Maalum ambavyo vitahusisha Wadau mbalimbali.