Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Usajili wa Vitambulisho vya Wafanyabiashara ndogondogo

  1. USAJILI WA VITAMBULISHO VYA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO

Zoezi  la  utambuzi  na  usajili  wa  wafanyabiashara  ndogondogo utasimamiwa  na  Mratibu  wa  Dawati  la  wafanyabiashara ndogondogo katika Halmashauri husika kwa kushirikiana na Afisa TEHAMA wa Halmashauri husika, Maafisa Biashara na Maafisa Maendeleo  ya  Jamii  katika  ngazi  mbalimbali  ikiwemo  Kata, viongozi wa Serikali katika ngazi ya Msingi (Mtaa/Kijiji) pamoja na viongozi wa wafanyabiashara ndogondogo. Maafisa Biashara na Maafisa  Maendeleo  ya  Jamii  katika  kila  ngazi  husika  wana dhamana  ya  kuhakiki,  kujiridhisha  na  kuthibitisha  taarifa  za anayesajiliwa  kwenye  mfumo  kuwa,  kweli  ni  mfanyabiashara ndogondogo aliyekusudiwa na Serikali kupatiwa kitambulisho hicho na si vinginevyo. Hivyo, endapo itatokea akasajiliwa mtu ambaye hausiki  kwenye  zoezi  hili,  Afisa  aliyemhakiki  na  kumthibitisha atalazimika kuwajibika kwa nafasi yake kisheria.

Kwa  msingi  huo,  mbali  na  uhakiki  wa  taarifa  muhimu  na kujiridhisha, ili mfanyabiashara ndogondogo aweze kutambuliwa na kusajiliwa kwenye mfumo huo atapaswa kuwa na sifa zifuatazo:-

i.    Awe  ni  mkazi  anayetambulika  na  uongozi  wa  Mtaa/Kijiji husika;

ii.    Awe na barua ya utambulisho kutoka kwenye Serikali ya Mtaa/Kijiji;

iii.    Awe   na   biashara   halali   inayotambulika   na   uongozi   wa wafanyabiashara wa Mtaa/Kijiji wa eneo hilo;

iv.    Awe na kitambulisho cha Taifa au Namba ya NIDA; na

v.    Aweze kulipa gharama ya Ada ya usajili.

 

Usajili wa Vitambulisho vya Wafanyabiashara ndogondogo