Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

HUDUMA KWA MANUSRA WA UKATILI  ZAIMARISHWA NCHINI.

Imewekwa: 17 Feb, 2025
HUDUMA KWA MANUSRA WA UKATILI  ZAIMARISHWA NCHINI.

Na WMJJWMM, Dodoma.

Serikali imeendelea kudhibiti ukatili dhidi ya wanawake na watoto kupitia afua mbalimbali ikiwemo Mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA) kwa kutoa huduama za afya kisaikolojia, kijami na kisheria kwa manusura

Hayo yamesemwa leo Februari 17,2025,Mkoani Dodoma na Kamishna msaidizi wa Ustawi wa Jamii, Tulo Masanja katika Kikao cha Utekelezaji  wa mpango wa  kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA) eneo la Huduma kwa Manusura wa Vitendo vya Ukatili.

Masanja amesema kuendelea kujitokeza kwa  vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ni  kiashiria hai kwamba  bado kuna uhitaji  wa kuimarisha  huduma kwa manusura  ikiwemo huduma za kiafya,Kisaikolojia na kisheria .

 “Licha ya serikali kufanikiwa kuimarisha huduma kwa watoto walio katika mazingira hatarishi, huduma za makazi ya Muda kwa manusra wa vitendo vya ukatili, kuwaaunganisha watoto na familia, Utoaji wa mafunzo ya huduma ya afya ya akili na msaada wa kisaikolojia na uimarishaji wa mifumo ya utoaji wa huduma, bado kuna  uelewa mdogo  kwa manusura kuhusu  haki za kijamii, kiuchumi na kisheria" amesema Masanja.

Kutokana na hali hiyo Serikali inaendelea kuelimisha jamii juu ya haki za wanawake na watoto, kwa kushirikiana na viongozi wa dini na mila ili kuhakikisha jamii inaachana na mila na desturi zenye madhara na kukuza utamaduni wa kulinda  haki za binadamu.

Aidha  mratibu wa dawati la  huduma za manusra wa ukatili  wa kijinsia kwa wanawake na watoto kutoka wizara ya Afya, Desteria Manyanga  amesema  huduma  zinazopatikana katika nyumba salama ni pamoja na kuwapatia dawa za kuzuia  maambukizi ya ukimwi au mimba endapo amebakwa na kuhakikisha manusura anapata matibabu  msaada wa kisaikolojia.

Kwa upande wake mwakilishi wa shirika linaloshughulika na masuala ya watoto (UNICEF) Tanzania, Evance Emori amesema shirika hilo linaendelea kushirikiana na serikali kuhakikisha kila mtoto analindwa na kupata haki zake za msingi.